Friday 27 June 2014

NAMNA YA KUPATA MCHUMBA

Kwa tafsiri isiyo rasmi mchumba ni mwanandoa mtarajiwa. Kabla ya kupata mchumba unapaswa kujua kanuni tatu (3) zinazohitajika katika mchakato wa kuwapata mchumba na hatimaye kuoa: -
1)   Maombi.
2)   Kutafuta.
3)   Kupata.

Naomba nifafanue kidogo kanuni hizo hapo juu:-
Maombi; Kila mwanadamu ana imani yake na kwa kupitia imani hiyo mahitaji yo yote ya muhimu kama chakula, malazi, mavazi, maisha marefu, mke mwema ni budi kumuomba yule tunayetegemea kwamba ndie mkuu na mwezeshaji wa mahitaji yetu yote (Mungu wako). Kwa hiyo, pia katika suala la kutafuta mchumba kuomba ni muhimu sana kwa maana hakuna jambo unaloweze kulipata binadamu pasipo kumuoomba Mungu wako.
Kutafuta; Baada ya kuomba kutokana na imani yako kinachofuata ni kutafuta yule mchumba uliyemuomba Mungu wako akupatie. Katika maombi yako lazima kuna wasifu unaotegemea awe nao huyo mchumba wako ambao umeomba Mungu wako akusaidie kukutafutia. Na kwa sababu Mungu wetu si mwanadamu atakupatia huyo mchumba unayemtafuta.
Kupata;
Baada ya kupata inatakiwa kuchunguza yafuatayo: -
1)   Sura yake na maumbile yake.
2)   Angalia ucha Mungu wake.
3)   Angalia tabia yake.
4)   Umri wake.
5)   Elimu yake.
6)   Fani yake.
7)   Ukoo wake.
Naomba nitoe ufafanuzi kidogo juu ya hayo mambo saba (7) yanayochunguzwa.
Sura yake na maumbile; Je, sura yake na maumbile yake yanaridhisha moyo wako? Kila binadamu hupendezwa na sura na maumbile fulani iwe mwanaume/mvulana au mwanamke/msichana. Kwa hiyo, katika hili kila mtu ana sifa anazopendelea.
Angalia ucha Mungu wake; Hapa cha kuangalia ni je, imani yake na yako ni sawa. Kama ni sawa ni vema kama si sawa je yuko tayari kujiunga na imani yako kwa roho moja na kwa dhati. Ikiwa ni hivyo ni vema, japo wengi utegeshea tu kwa lengo la kufunga ndoa na hatimaye urudia tena imani zao zamani.
Angalia tabia yake; Hapa ni kuangalia je, tabia yake inakuridhisha na inakupendeza kuwa mwenzi wako wa maisha. Kama jibu ni ndio weka vema. Kama jibu ni siyo je, anarekebishika. Kama jibu ni ndiyo jaribu kumrekebisha ukifanikiwa ni vema, chukua hatua.
Umri wake; Hapa chakuangalia ni je! umri mko sawa au amekuzidi? Kama mko sawa au amekuzidi wataalamu wa mambo ya ndoa huwa wanashauri si vizuri kwa mwanaume kuoana na mwanamke aliye mzidi kwa sababu wanawake wana kawaida ya kuzeeka haraka kwa hiyo baada ya zao kadhaa ataonekana ni mzee sana kuliko wewe. Wataalamu wa mambo ya ndoa ushauri mwanaume awe na umri mkubwa kuliko mwanamke kwa miaka kadhaa hata miaka kumi (10) ni sawa tu.
Elimu yake; Ki-elimu ni muhimu sana kuwa na tofauti ndogo sana miongoni mwao au wakawa na elimu sawa. Hii, ni muhimu sana ili kutokuwepo tofauti kubwa ya kiuelewa wa mambo mbalimbali katika jamii na urahisi wa kujichanganya katika jamii.
Fani yake; Kwa tafsiri Fani ni kazi yake inayomfanya aendeshe maisha yake kama vile uandisi, uhasibu, nesi, mwalimu, fundi cherehani; mfanyabiashara nakadhalika. Ni muhimu kujua fani yake ili kujua kama itashabihiana vipi na yako kwa mustakabali wa maisha yenu ya siku za usoni. Kama fani yake haitaleta shida upande wa malezi ya mahusiano yenu ni vema.
Ukoo/Familia wake/yake; Kwa tafsiri ya ukoo ni babu/bibi, vituku nakadhalika walikuwa na magonjwa gani ya kuridhi. Ili kwa maisha ya sasa limekuwa ni gumu sana kwa sababu ya jamii nyingi kutokuwa na mipaka katika masuala ya kuoana.
Iwapo katika vipengere hivyo saba (7) kama vitatu (3) mpaka vine (4) viko sawa ni vema ukachukua hatua ya kuoa kwa maana mambo mengine yanarekebishika mkiwa ndani ya ndoa.
Hongera kwa kuwa mwanachama wa wavuti hii, nakuomba uwaalike wenzako na ndugu zako. Nakaribisha ushauri na maoni kwa kupitia wavuti hii au kwa njia ya simu 0719841988 au 0784190882.


Monday 23 June 2014

SIFA 14 ZA MME NA MKE BORA

MME BORA
Ahsante sana msomaji kwa kuamua kujiunga na Blogu hii awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipatia uzima na ufahamu mpaka kuniwezesha kuandika machache kuhusu mada ya leo inayosomeka sifa za mwanaume bora aliyeoa.
Sifa husika ni kama zifuatazo: -
? Mcha Mungu.
? Anampenda mkewe.
? Anamheshimu mkewe.
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi.
? Uwathamini ndugu wa mkewe sawa na ndugu zake.
? Anajua kumlinda/kumtunza mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mkewe.
? Uomba ushauri kwa mkewe katika maamuzi muhimu ya kifamilia
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kiume.

MKE BORA

Sifa hizo ni kama zifuatavyo:-
? Mcha Mungu.
? Anampenda mmewe.
? Anamheshimu mmewe
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi wa mwili na anahakikisha nyumba ni safi muda wote.
? Uwathamini ndugu wa mmewe sawa na ndugu zake
? Anajua kumlinda/kumtunza/kufundisha mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mmewe.
? Ni mshauri mkuu wa mmewe.
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea.
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kike.
Sifa zote za mwanaume na mwanamke zinafanana kasoro kwenye kipengere cha usafi upande wa mwanamke kuna maneno yameongezeka kidogo ya msisitizo.


Thursday 22 May 2014

NAMNA YA KUKABILIANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA WANANDOA WENYEWE

Kama nilivyoeleza kwenye makala yangu ya changamoto zinazosababishwa na wanadoa wenye mmojawapo ni mawasiliano(kutokuelewana). Hii ndio changamoto(migogoro) kubwa sana katika ndoa na ndio chanzo cha taraka nyingi kwa mujibu takwimu za kimataifa. Kwa mbaya tarakwimu za hapa kwetu nimeshindwa kuzipata kwa njia ya vyanza vyangu.
Kimsingi ni kwamba migogoro inayosababishwa na kutoelewana chanzo chake kinaweza kuwa ni mmoja wa wanadoa au wote wawili. Migogoro kikawaida ipo kwenye ndoa zote ila hutofautiana kwa kiwango. Ipo kwenye kila ndoa kutokana na sababu za malezi na tabia za asili za wanandoa. Na kawaida migogoro ukua kutokana na kukosa utayari wa kuitatua kwa wanandoa wenyewe wote wawili au mmoja wao. Inapotokea hakuna utayari kwa wote wawili ndoa haiwezi kudumu na kama ni kwa mmoja kuna asilimia fulani ndoa kuweza kudumu na kama wote wako tayari kutatua ndoa hii inakuwa na asilimia 100 kudumu.
Kama nilivyoongea kwenye makala tajwa hapo juu. Migogoro ya kutoelewana ipo inayotokana na mahitaji ya kawaida na ya kimwili. Ninavyosema mahitaji ya kawaida ni nina maana mahitaji ya msingi ya binadamu ni chakula na mavazi na mengine ambayo siyo msingi yaani; mahitaji ya kumpendezesha mwanandoa, kushaurishwa, kuthaminiwa n.k.
NAMNA YA KUPAMBANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KAWAIDA
1.    Kuwa mkweli kuhusu hali ya kipato chako.
Kuwa mkweli wa hali yako ki-uchumi yaani; kuwa mkweli kwa mwenza wako kuhusu hali ya mapato yako. Na ukweli huu ni vizuri ufanyike kabla ya kufunga ndoa. Ni vizuri sana kama utauvaa uhalisia wako kimapato kipindi chote cha uchumba. Hili, ni muhimu sana kwa sababu ikusaidia kujua kama mchumba wako ni wa kiwango chako au la. Ukidanganya katika suala hili unakuwa umepande mgogoro ambayo itakuwa vigumu kuusuluhisha na unakuwa umejenga hali ya kutoaminika. Kwenye maelezo haya nichukulia ndoa yenye kutegemea kipato cha mwnandoa mmoja.
Pia hata pale ambapo wanandoa wote wanakipato, ni vizuri wanandoa wakawa wanajuana vipatavyo wote kwa urahisi ya kupanga mipango yao ya maendeleo kwa pamoja yenye kulingana na kipato chao.
2.    Onyesha kujali hitaji la mwenza wako.
Jitahidi kujali mahitaji ya mwenza wako kwa kumtimizia hitaji lake kama uwezo unaruhusu na kama unaona sihitaji la msingi, tafuta lugha nzuri ya kumweleza ni kwa nini unaona hitaji lisitimizwe na bila kuonyesha dalili za kupuuza au kuonyesha sihitaji la msingi.
3.    Epuka kuonyesha upendeleo katika kusaidia ndugu.
Katika familia zetu za ki-afrika kuna matatizo ya kila namna kwenye familia zetu yaani; kwa upande wa mke na mwanaume. Inapotokea kuna mahitaji upande wa familia za upande mmojawapo ni muhimu sana kuweka uwiano wa misaada inayotolea, ili kuepuka kuonyesha upendeleo.
4.    Epuka kuonyesha upendeleo kwa wageni wanao watembelea nyumbani.
Ni jambo la kawaida sana ndugu wa pande zote kutamani kuwatembelea wanandoa katika hali ya amani au matatizo. Ni vizuri kujitahidi kutoonyesha unyanyapaa kwa wanandugu wa upande mmoja hali hii inaweza kuleta mgogoro mkuu.
5.    Epuka kuonyesha dharau dhidi ya mila na desturi za mwenzi wako.
Inapotokea wanandoa ni makabila tofauti ina maana watakuwa wamekulia kataika mila na desturi tofauti. Mila na desturi uhusisha namna ya kuongea, mapishi, tofauti za ki-maendeleo baina ya kabila moja na nyingine. Si vizuri kuonyesha dharau hata kama ni katika hali ya utani kwa sababu hiyo huonyesha hisia zako dhidi ya mwenzako hata kama utasema unamtania.
6.    Epuka utani unaoeleka kweli uhalisia kimaumbile.
Jitahidi kuepuka utani unaohusiana na maumbile kama vile watu wafupi au wanene wana kasoro 1,2,3 n.k. wakati ukijua kwamba mwenza wako nao ana maumbile kama hayo. Utani kama huo hufanya mtaniwa kujisikia vibaya na kuleta migogoro katika ndoa.
7.    Kushaurishwa katika mambo ya msingi ki-familia.

Kitabia kila binadamu anapenda kuthaminiwa katika mambo tofauti tofauti kama kazi zake, ushauri n.k. Katika mambo ni pamoja na katika mambo ya msingi ya maendeleo ya kifamilia kama vile ununuzi wa kitu cho chote cha kifamilia kama vile samani, na vitu vingine muhimu katika maisha yetu ya kila siku.
 NAMNA YA KUTATUA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KIMWILI
Katika jamii zetu, mgogoro huu ni mkubwa sana kwa sababu takwimu zinavyoonyesha wanandoa wengi wanatoka nje ya ndoa. Takwimu hizi ni takwimu za maambulizi ya virusi vya UKIMWI. Sijafanya jitihada ya kutafuta takwimu hizi kwa sababu si jambo muhimu sana katika makala hii.

Katika hitaji hili utatuzi wake hutegemea sana mambo yafuatayo:-

ü  Uwazi wa hisia
ü  Utayari wa kujua mwili wa mwenza wako
ü  Na uwezo wake wa mwenza wako
ü  Kiwango chake cha uhitaji wake n.k.

Kifupi ni kwamba jambo hili la faragha halina kanuni maalum kwa sababu pia kuna migogoro inayotokana suala la kimaumbile, vyakula, kazi n.k.

Msingi imara wa ndoa yo yote unakuwa imara unapojengwa katika msingi ya kumtegemea Mungu kuwa kiongozi na mshauri mkuu katika ndoa.

Karibu sana UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA kwa kuondoa migogoro isiyo ya lazima katika familia zetu.