Friday 27 June 2014

NAMNA YA KUPATA MCHUMBA

Kwa tafsiri isiyo rasmi mchumba ni mwanandoa mtarajiwa. Kabla ya kupata mchumba unapaswa kujua kanuni tatu (3) zinazohitajika katika mchakato wa kuwapata mchumba na hatimaye kuoa: -
1)   Maombi.
2)   Kutafuta.
3)   Kupata.

Naomba nifafanue kidogo kanuni hizo hapo juu:-
Maombi; Kila mwanadamu ana imani yake na kwa kupitia imani hiyo mahitaji yo yote ya muhimu kama chakula, malazi, mavazi, maisha marefu, mke mwema ni budi kumuomba yule tunayetegemea kwamba ndie mkuu na mwezeshaji wa mahitaji yetu yote (Mungu wako). Kwa hiyo, pia katika suala la kutafuta mchumba kuomba ni muhimu sana kwa maana hakuna jambo unaloweze kulipata binadamu pasipo kumuoomba Mungu wako.
Kutafuta; Baada ya kuomba kutokana na imani yako kinachofuata ni kutafuta yule mchumba uliyemuomba Mungu wako akupatie. Katika maombi yako lazima kuna wasifu unaotegemea awe nao huyo mchumba wako ambao umeomba Mungu wako akusaidie kukutafutia. Na kwa sababu Mungu wetu si mwanadamu atakupatia huyo mchumba unayemtafuta.
Kupata;
Baada ya kupata inatakiwa kuchunguza yafuatayo: -
1)   Sura yake na maumbile yake.
2)   Angalia ucha Mungu wake.
3)   Angalia tabia yake.
4)   Umri wake.
5)   Elimu yake.
6)   Fani yake.
7)   Ukoo wake.
Naomba nitoe ufafanuzi kidogo juu ya hayo mambo saba (7) yanayochunguzwa.
Sura yake na maumbile; Je, sura yake na maumbile yake yanaridhisha moyo wako? Kila binadamu hupendezwa na sura na maumbile fulani iwe mwanaume/mvulana au mwanamke/msichana. Kwa hiyo, katika hili kila mtu ana sifa anazopendelea.
Angalia ucha Mungu wake; Hapa cha kuangalia ni je, imani yake na yako ni sawa. Kama ni sawa ni vema kama si sawa je yuko tayari kujiunga na imani yako kwa roho moja na kwa dhati. Ikiwa ni hivyo ni vema, japo wengi utegeshea tu kwa lengo la kufunga ndoa na hatimaye urudia tena imani zao zamani.
Angalia tabia yake; Hapa ni kuangalia je, tabia yake inakuridhisha na inakupendeza kuwa mwenzi wako wa maisha. Kama jibu ni ndio weka vema. Kama jibu ni siyo je, anarekebishika. Kama jibu ni ndiyo jaribu kumrekebisha ukifanikiwa ni vema, chukua hatua.
Umri wake; Hapa chakuangalia ni je! umri mko sawa au amekuzidi? Kama mko sawa au amekuzidi wataalamu wa mambo ya ndoa huwa wanashauri si vizuri kwa mwanaume kuoana na mwanamke aliye mzidi kwa sababu wanawake wana kawaida ya kuzeeka haraka kwa hiyo baada ya zao kadhaa ataonekana ni mzee sana kuliko wewe. Wataalamu wa mambo ya ndoa ushauri mwanaume awe na umri mkubwa kuliko mwanamke kwa miaka kadhaa hata miaka kumi (10) ni sawa tu.
Elimu yake; Ki-elimu ni muhimu sana kuwa na tofauti ndogo sana miongoni mwao au wakawa na elimu sawa. Hii, ni muhimu sana ili kutokuwepo tofauti kubwa ya kiuelewa wa mambo mbalimbali katika jamii na urahisi wa kujichanganya katika jamii.
Fani yake; Kwa tafsiri Fani ni kazi yake inayomfanya aendeshe maisha yake kama vile uandisi, uhasibu, nesi, mwalimu, fundi cherehani; mfanyabiashara nakadhalika. Ni muhimu kujua fani yake ili kujua kama itashabihiana vipi na yako kwa mustakabali wa maisha yenu ya siku za usoni. Kama fani yake haitaleta shida upande wa malezi ya mahusiano yenu ni vema.
Ukoo/Familia wake/yake; Kwa tafsiri ya ukoo ni babu/bibi, vituku nakadhalika walikuwa na magonjwa gani ya kuridhi. Ili kwa maisha ya sasa limekuwa ni gumu sana kwa sababu ya jamii nyingi kutokuwa na mipaka katika masuala ya kuoana.
Iwapo katika vipengere hivyo saba (7) kama vitatu (3) mpaka vine (4) viko sawa ni vema ukachukua hatua ya kuoa kwa maana mambo mengine yanarekebishika mkiwa ndani ya ndoa.
Hongera kwa kuwa mwanachama wa wavuti hii, nakuomba uwaalike wenzako na ndugu zako. Nakaribisha ushauri na maoni kwa kupitia wavuti hii au kwa njia ya simu 0719841988 au 0784190882.


Monday 23 June 2014

SIFA 14 ZA MME NA MKE BORA

MME BORA
Ahsante sana msomaji kwa kuamua kujiunga na Blogu hii awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipatia uzima na ufahamu mpaka kuniwezesha kuandika machache kuhusu mada ya leo inayosomeka sifa za mwanaume bora aliyeoa.
Sifa husika ni kama zifuatazo: -
? Mcha Mungu.
? Anampenda mkewe.
? Anamheshimu mkewe.
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi.
? Uwathamini ndugu wa mkewe sawa na ndugu zake.
? Anajua kumlinda/kumtunza mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mkewe.
? Uomba ushauri kwa mkewe katika maamuzi muhimu ya kifamilia
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kiume.

MKE BORA

Sifa hizo ni kama zifuatavyo:-
? Mcha Mungu.
? Anampenda mmewe.
? Anamheshimu mmewe
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi wa mwili na anahakikisha nyumba ni safi muda wote.
? Uwathamini ndugu wa mmewe sawa na ndugu zake
? Anajua kumlinda/kumtunza/kufundisha mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mmewe.
? Ni mshauri mkuu wa mmewe.
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea.
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kike.
Sifa zote za mwanaume na mwanamke zinafanana kasoro kwenye kipengere cha usafi upande wa mwanamke kuna maneno yameongezeka kidogo ya msisitizo.