Friday 19 May 2017

MAZOEA SABA (7) MABAYA KWA WANANDOA

Napenda tena kuchukua nafasi hii adimu kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipa nafasi ya kuwasilisha kwenu baadhi ya mazoea mabaya ustawi ndoa ambayo hufanywa na wanandoa wengi. Pia napenda kuwashukuru wale wote waliopata nafasi ya kusoma makala zangu kwa maoni na mawazo yenu mazuri, napenda kuchukua nafasi hii kuwaombeni mwaalike na wenzenu kusoma makala zangu ambazo huwa natoa kila wiki.
Leo nitaongelea makosa saba (7) ambayo mara nyinyi hufanywa na wanandoa na kusababisha kuibuka kwa migogoro katika mahusiano. Makosa hayo ni kama yafuatavyo: -
1.   Kususia tendo la ndoa bila sababu ya msingi; Tendo la ndoa ni mmojawapo wa nguzo muhimu ya ndoa zote. Kwa hiyo, inapotokea mmoja wa wanandoa kuamua kumnyima mwenzake tendo la ndoa bila sababu ya msingi ni tendo ambalo linaweza kusababisha kuvunjika kwa ndoa bila kujali ni ya kidini, kimila au kiserikali.
2.   Kumsema vibaya mwenzako wako kwa rafiki/ndugu; Ni makosa makubwa sana kwa mustakabali wa ndoa kwa mmoja wa wanandoa kumsema vibaya mwenzake kwa rafiki zake au ndugu zake badala ya kumuelimisha ili kuondoa  kasoro unazoziona kwake.
3.   Kutotimiza yale unayosema; Ni kosa kubwa sana kwa mwanandoa kutotimiza/kutenda yale anayoahidi kwa mkewe/mmewe bila sababu ya msingi. Katika mahusiano hutokea misukosuko ya hapa na pale na nyingi hutokea mmoja wa wanandoa kuomba msamaha na kukiri kutorudia vitendo fulani ambavyo ni kero kwa mwenzako kwa mfano; kulala nje, kuchelewa kurudi nyumbani bila taarifa yo yote, nakadhalika.
4.   Kutokukubali makosa; Ni busara kwa mstakabali mzuri wa ndoa kukubali makosa inapotokea kuwa mmoja wa wanandoa kafanya makosa. Imekuwa ni vigumu sana kwa wanandoa hasa wanaume kukubali makosa inapotokea wamefanya makosa na badala yake huonyesha kukiri kwa vitendo yaani; kufuata mapendekezo ya wake zao na siyo kukubali kwamba maamuzi yao ya awali yalikuwa na makosa. Si dhambi kukiri kufanya maamuzi kimakosa inapotokea kwa mustakabali mwema wa mahusiano.
5.   Kuwa na hasira zisizo na mpangilio; Ni makosa makubwa kuwa na hasira zisizo na mpangilio kwa mwenzako au kuhamisha hasira kutoka ofisini au kwenye shughuli yo yote unayoifanya na kuzipeleka nyumbani.
Nyumbani ni mahali ambapo inakiwa iwe ni pakupatia faraja na pumziko stahili.
6.   Kutojishughulisha na kumuelewa mwenzako; Ni jambo jema kwa mustakabali mzuri mahusiano kufanya jitihadi kumuelewa mwenzako anakuweje katika hali ya furaha au huzuni. Hili ni muhimu sana katika mahusiano hata katika urafiki wa kawaida. Hii ni nguzo muhimu sana katika kudumisha mahusiano kwa wanandoa. Kinyume cha hapo ni kujenga mifarakano isiyo lazoma.
7.   Kutomshukuru mwenzako anapokuwa amefanya jambo zuri; Ni vizuri inapotokea mwanaume/mwanamke kafanya jambo jema kumshukuru ili kumpa moyo wa kufanya vizuri zaidi siku nyingine. Kwa mfano kama mwanaume/mwanamke ameamua kwa upendo kukununulia zaidi ya nguo ni busara kumshukuru kwanza kwa zawadi hiyo badala ya kulaumiwa kwamba nguo hiyo siyo nzuri au imeshapitwa na wakati, umeuziwa bei mbaya, karudishe nakadhalika.
Mambo yote hayo niliyoyataja hapo juu yanaweza kuepukwa, iwapo utakuwa mtafiti  na utamweka Mungu karibu  katika maisha yako yote.  Na pia kwa ushauri naomba tuwasilianae kwa barua pepe ya fkmwamoto@gmail.com  kwa ushauri makini wa masuala ya mahusiano.