Wednesday 3 January 2018

MAHUSIANO KWA MWAKA 2018

Leo ni siku ya tatu(3) tangu tuanze mwaka 2018, ili kudumisha na kuboresha mahusiano yetu kwa mwaka huu mpya. Napenda kuwashauri kuishia kwa kanuni zifuatazo: -
©       Kuacha kuangalia madhaifu kwa mwenza wako, bali tuangalie mazuri ya mwenza wako.
©       Tumuombe Mungu atupe uwezo wa kusamehe, ili maombi yetu yaweze kupokelewa na Mungu wetu
©       Kuepuka kushirikisha watu wengi kwenye husiano wetu bali tumshirikishe Mungu msimamizi na muasisi wa uhusiano na ndoa.
©       Jitahidi kuwaelewa wenzetu badala ya kutaka wenzetu kutuelewa sisi.
©       Tuheshimu matumizi ya muda kwa maana ni raslimali muhimu sana katika maisha yetu.
©       Shirikiana na kila mtu unayekutana naye kwa maana kila mwanadamu ni muhimu kwako kama siyo kwa leo ni kwa siku za baadae.

Naomba kwa leo tuishie hapo.