Leo ni siku ya tatu(3) tangu tuanze mwaka 2018, ili
kudumisha na kuboresha mahusiano yetu kwa mwaka huu mpya. Napenda kuwashauri
kuishia kwa kanuni zifuatazo: -
©
Kuacha kuangalia madhaifu kwa mwenza wako, bali
tuangalie mazuri ya mwenza wako.
©
Tumuombe Mungu atupe uwezo wa kusamehe, ili
maombi yetu yaweze kupokelewa na Mungu wetu
©
Kuepuka kushirikisha watu wengi kwenye husiano
wetu bali tumshirikishe Mungu msimamizi na muasisi wa uhusiano na ndoa.
©
Jitahidi kuwaelewa wenzetu badala ya kutaka
wenzetu kutuelewa sisi.
©
Tuheshimu matumizi ya muda kwa maana ni
raslimali muhimu sana katika maisha yetu.
©
Shirikiana na kila mtu unayekutana naye kwa
maana kila mwanadamu ni muhimu kwako kama siyo kwa leo ni kwa siku za baadae.
Naomba kwa leo tuishie hapo.