1. Kwanza kabisa, tunasamehe kwa sababu kusamehe ni amri na ni agizo la Mungu.
binadamu ni watu ambao hawapendi kukubali kosa ni watu waliozoea kujitetea na
kukataa kosa pale anapokosa. Kama tukikataa kutii tunakaidi agizo la Mungu
hivyo tunapaswa kusameheana kwani muasisi wa msamaha ni Mungu mwenyewe na kama
Mungu angehesabu maovu yetu nani angesimama? Anza leo kusamehe, hakuna aliye
mkamilifu.
2. Tunasamehe ili tuweze
kusamehewa na pia ili maombi yetu yaweze kupokelewa na Mwenyezi Mungu. Unapaswa
kusamehe kwa faida yako mwenyewe siyo kwa faida ya mkosaji na mwachie Mungu
apambane na watesi wako wala usilipe kisasi wewe mwekee mtesi wako kaa la moto
kichwani limchome. Kumwekea kaa la moto kichwani ni kama kumtesa kisakikolojia
wewe unamsamehe yeye, amini basi nafsi yake inaendelea kumtafuna.
3. Unasamehe ili uwe na Amani
ya moyoni mwako. Unaposamehe unakuwa unapata amani ya moyo. Mtu ambaye
anavumilia uchungu ulioumbika ndani ya moyo na hataki kuachilia fundo hilo
lazima litamtesa na atakosa amani ya moyo. Atahangaika na huku uchungu
ulioumbika ndani ya moyo ukiendelea kumtafuta.
4. Unasamehe ili uwe na furaha
moyoni mwako. Kwa kweli ukiangalia watu wanaokataa kusameheana huwa hawana
furaha kabisa katika mioyo yao. Kama unaishi katika mahusiano yoyote na mara
nyingi huwa watu si wakamilifu basi msamaha ndio kiunganishi chenu ambao
utarudisha uhusiano uliopotea au uliovunjika na kuleta uhusiano wa awali yaani
uhusiano mpya.
5. Tunasamhe ili
tuwe na afya njema. Uponyaji wa kweli unaanzia moyoni. Kama mtu anasamehe
kutoka moyoni basi huo ni msamaha wa kweli na ni msamaha unaongozwa na huruma
ya Mungu ndani yake. Watu hawataki kusamehe ndio maana wengine afya zao ni
dhaifu. Uchungu ulioumbika ndani ya moyo unaendelaa kumtafuna. Usizeeke kabla
ya wakati kwa ajili ya kutosamhe.
6. Kutosamhe kunakufanya
ujikinai wewe mwenyewe. Unajiona wewe ni mtu ambaye hustahili kuwepo hapa
duniani. Utajiona wewe hauna maana hapa duniani utakua unakaa peke yako peke
yako. Huna furaha, amani, upendo. Maisha yako yanakuwa yamejaa sumu na majeraha
moyoni ugonjwa umekuwa mkubwa na wewe hutaki kuupatia dawa ya kuuponya na dawa
yake ni msamaha tu.
7. Kutokusamhe
kunaongeza maadui katika maisha yako. Kuna faida kubwa sana ya kusamehe. Jaribu
kuangalia katika maisha yako Yule anayesamehe na asiyesamehe nani anakuwa
anaongeza maadui? Utaongeza maadui na utavunja uhusiano na watu hivyo utakua
unaishi maisha ya umimi. Maisha ya binadamu ni maisha yenye uhusiano kama
husamehi basi unajitengenezea duniani yako mwenyewe.
8. Kutosamhe kunaleta
mapasuko wa kifamilia. Katika hali ya kawaida jaribu kuangalia katika jamii
yako ni familia ngapi zimesambaratika kwasababu ya kutosameheana ? ni nyingi
sana kwanza familia nyingi zina migogoro ya aina mbalimbali inayosababishwa na
watu kulipiana visasi na kutosameheana na kuishi maisha ya chuki kama ya paka
na panya. Kusamehe ni faida kwa kila familia bora inayotaka amani na furaha,
mipasuko katika familia itaendela kuwepo kama watu wasiposameheana.
9. Kutosamhe kunaleta unyonge
wa moyo yaani huzuni. Ukiwaangalia watu wengine unawaonea huruma wanaishi
maisha ya huzuni wakati falsafa ya maisha ni furaha hapa duniani. Tunatafuta
kila siku ili tuweze kuwa na furaha. Inuka leo na nenda kazike hilo jeneza la
huzuni na kuwa huru na maisha yako. Huoni ni utumwa kuwabeba watu moyoni?
Hujaja duniani kuteseka na maisha ni mafupi sana samehe na endelea na maisha
yako.
10. Kutosamhe kunawafanya
watu kukimbia makazi na ofisi zao. Kwa mfano, watu waliokoseana na hawataki
kusameheana huwa wanaishi maisha kama ya paka na panya. Akimuona mwenzake huyo
anakuja anakimbia kama yuko nyumbani anakimbia, kama ni njia anabadilisha
kabisa ili wasionane na kusalimiana. Unakuta watu wengine wanakimbia kabisa
ofisi zao kwa sababu ya kutotaka kusameheana. Kwanini uendelea kuishi maisha
haya? Anza kubadilika kama ulikuwa unakimbia makazi au ofisi ili usikutane na
mtesi wako.Maisha ya kutokusamehe yanahasara nyingi na faida ni nyingi zaidi kuliko hasara. Imani za watu zinakufa kwa ajili ya kutokusamehe, watu wanazeeka mapema kabla ya muda, watoto wa mitaani wanaongezeka kwa ajili ya kutokusamehe yaani; pale wazazi wanapotalakiana na kuwatelekeza watoto. Tuishi katika maisha ya kusameheana na siyo ya kulipizana visasi.
Kwa ushauri tuwasiliane kwa barua-pepe fkmwamoto@gmail.com au Whatsapp 0784190882