Thursday 22 May 2014

NAMNA YA KUKABILIANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA WANANDOA WENYEWE

Kama nilivyoeleza kwenye makala yangu ya changamoto zinazosababishwa na wanadoa wenye mmojawapo ni mawasiliano(kutokuelewana). Hii ndio changamoto(migogoro) kubwa sana katika ndoa na ndio chanzo cha taraka nyingi kwa mujibu takwimu za kimataifa. Kwa mbaya tarakwimu za hapa kwetu nimeshindwa kuzipata kwa njia ya vyanza vyangu.
Kimsingi ni kwamba migogoro inayosababishwa na kutoelewana chanzo chake kinaweza kuwa ni mmoja wa wanadoa au wote wawili. Migogoro kikawaida ipo kwenye ndoa zote ila hutofautiana kwa kiwango. Ipo kwenye kila ndoa kutokana na sababu za malezi na tabia za asili za wanandoa. Na kawaida migogoro ukua kutokana na kukosa utayari wa kuitatua kwa wanandoa wenyewe wote wawili au mmoja wao. Inapotokea hakuna utayari kwa wote wawili ndoa haiwezi kudumu na kama ni kwa mmoja kuna asilimia fulani ndoa kuweza kudumu na kama wote wako tayari kutatua ndoa hii inakuwa na asilimia 100 kudumu.
Kama nilivyoongea kwenye makala tajwa hapo juu. Migogoro ya kutoelewana ipo inayotokana na mahitaji ya kawaida na ya kimwili. Ninavyosema mahitaji ya kawaida ni nina maana mahitaji ya msingi ya binadamu ni chakula na mavazi na mengine ambayo siyo msingi yaani; mahitaji ya kumpendezesha mwanandoa, kushaurishwa, kuthaminiwa n.k.
NAMNA YA KUPAMBANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KAWAIDA
1.    Kuwa mkweli kuhusu hali ya kipato chako.
Kuwa mkweli wa hali yako ki-uchumi yaani; kuwa mkweli kwa mwenza wako kuhusu hali ya mapato yako. Na ukweli huu ni vizuri ufanyike kabla ya kufunga ndoa. Ni vizuri sana kama utauvaa uhalisia wako kimapato kipindi chote cha uchumba. Hili, ni muhimu sana kwa sababu ikusaidia kujua kama mchumba wako ni wa kiwango chako au la. Ukidanganya katika suala hili unakuwa umepande mgogoro ambayo itakuwa vigumu kuusuluhisha na unakuwa umejenga hali ya kutoaminika. Kwenye maelezo haya nichukulia ndoa yenye kutegemea kipato cha mwnandoa mmoja.
Pia hata pale ambapo wanandoa wote wanakipato, ni vizuri wanandoa wakawa wanajuana vipatavyo wote kwa urahisi ya kupanga mipango yao ya maendeleo kwa pamoja yenye kulingana na kipato chao.
2.    Onyesha kujali hitaji la mwenza wako.
Jitahidi kujali mahitaji ya mwenza wako kwa kumtimizia hitaji lake kama uwezo unaruhusu na kama unaona sihitaji la msingi, tafuta lugha nzuri ya kumweleza ni kwa nini unaona hitaji lisitimizwe na bila kuonyesha dalili za kupuuza au kuonyesha sihitaji la msingi.
3.    Epuka kuonyesha upendeleo katika kusaidia ndugu.
Katika familia zetu za ki-afrika kuna matatizo ya kila namna kwenye familia zetu yaani; kwa upande wa mke na mwanaume. Inapotokea kuna mahitaji upande wa familia za upande mmojawapo ni muhimu sana kuweka uwiano wa misaada inayotolea, ili kuepuka kuonyesha upendeleo.
4.    Epuka kuonyesha upendeleo kwa wageni wanao watembelea nyumbani.
Ni jambo la kawaida sana ndugu wa pande zote kutamani kuwatembelea wanandoa katika hali ya amani au matatizo. Ni vizuri kujitahidi kutoonyesha unyanyapaa kwa wanandugu wa upande mmoja hali hii inaweza kuleta mgogoro mkuu.
5.    Epuka kuonyesha dharau dhidi ya mila na desturi za mwenzi wako.
Inapotokea wanandoa ni makabila tofauti ina maana watakuwa wamekulia kataika mila na desturi tofauti. Mila na desturi uhusisha namna ya kuongea, mapishi, tofauti za ki-maendeleo baina ya kabila moja na nyingine. Si vizuri kuonyesha dharau hata kama ni katika hali ya utani kwa sababu hiyo huonyesha hisia zako dhidi ya mwenzako hata kama utasema unamtania.
6.    Epuka utani unaoeleka kweli uhalisia kimaumbile.
Jitahidi kuepuka utani unaohusiana na maumbile kama vile watu wafupi au wanene wana kasoro 1,2,3 n.k. wakati ukijua kwamba mwenza wako nao ana maumbile kama hayo. Utani kama huo hufanya mtaniwa kujisikia vibaya na kuleta migogoro katika ndoa.
7.    Kushaurishwa katika mambo ya msingi ki-familia.

Kitabia kila binadamu anapenda kuthaminiwa katika mambo tofauti tofauti kama kazi zake, ushauri n.k. Katika mambo ni pamoja na katika mambo ya msingi ya maendeleo ya kifamilia kama vile ununuzi wa kitu cho chote cha kifamilia kama vile samani, na vitu vingine muhimu katika maisha yetu ya kila siku.
 NAMNA YA KUTATUA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KIMWILI
Katika jamii zetu, mgogoro huu ni mkubwa sana kwa sababu takwimu zinavyoonyesha wanandoa wengi wanatoka nje ya ndoa. Takwimu hizi ni takwimu za maambulizi ya virusi vya UKIMWI. Sijafanya jitihada ya kutafuta takwimu hizi kwa sababu si jambo muhimu sana katika makala hii.

Katika hitaji hili utatuzi wake hutegemea sana mambo yafuatayo:-

ü  Uwazi wa hisia
ü  Utayari wa kujua mwili wa mwenza wako
ü  Na uwezo wake wa mwenza wako
ü  Kiwango chake cha uhitaji wake n.k.

Kifupi ni kwamba jambo hili la faragha halina kanuni maalum kwa sababu pia kuna migogoro inayotokana suala la kimaumbile, vyakula, kazi n.k.

Msingi imara wa ndoa yo yote unakuwa imara unapojengwa katika msingi ya kumtegemea Mungu kuwa kiongozi na mshauri mkuu katika ndoa.

Karibu sana UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA kwa kuondoa migogoro isiyo ya lazima katika familia zetu.


No comments:

Post a Comment