Monday 23 June 2014

SIFA 14 ZA MME NA MKE BORA

MME BORA
Ahsante sana msomaji kwa kuamua kujiunga na Blogu hii awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipatia uzima na ufahamu mpaka kuniwezesha kuandika machache kuhusu mada ya leo inayosomeka sifa za mwanaume bora aliyeoa.
Sifa husika ni kama zifuatazo: -
? Mcha Mungu.
? Anampenda mkewe.
? Anamheshimu mkewe.
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi.
? Uwathamini ndugu wa mkewe sawa na ndugu zake.
? Anajua kumlinda/kumtunza mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mkewe.
? Uomba ushauri kwa mkewe katika maamuzi muhimu ya kifamilia
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kiume.

MKE BORA

Sifa hizo ni kama zifuatavyo:-
? Mcha Mungu.
? Anampenda mmewe.
? Anamheshimu mmewe
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi wa mwili na anahakikisha nyumba ni safi muda wote.
? Uwathamini ndugu wa mmewe sawa na ndugu zake
? Anajua kumlinda/kumtunza/kufundisha mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mmewe.
? Ni mshauri mkuu wa mmewe.
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea.
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mmewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kike.
Sifa zote za mwanaume na mwanamke zinafanana kasoro kwenye kipengere cha usafi upande wa mwanamke kuna maneno yameongezeka kidogo ya msisitizo.


No comments:

Post a Comment